SOMA UNAJUA KWANINI HUJIBIWI HATA KUBADILISHWA KIROHO NA KIMWILI

SOMO🎤🎤Ijue Madhabahu ilivyo na Majibu yako ukisimama Nayo

✍️✍️Leo Tunataka Tujifunze Madhabahu Njisi ilivyo na nguvu ya KUKUFANYA upokee majibu au Usipokee
Tufunue Biblia Zetu Tusome Vitabu hivi 👉👉1wafalme;18;25-32✍️Kutoka:20;26, 24:4,29;37 Mathayo;5;20_26

                 ✍️✍️✍️ UTANGULIZI ✍️✍️✍️
Madhabahu huwa Ni Mahusiano yanayompatia uhalali mtu wa Kupokea au Asipokee kumtambulisha mtu Anamuwakilisha Mungu au Shetani Pia Madhabahu huwa Ni Kitu kilichomo ndani ya Mtu Yenye uwezo wa Kutenda vitu kwa wakati na kwa watu husika wanaoendana Pamoja na ile Madhabahu Mchungaji Kama Hana Madhabahu inayoongea kwa Habari ya Tatizo lako hata akuombee vipi huwezi kufunguliwa mpaka ukutane na Madhabahu yako itabadili historia
Tusome hadhi hii 1 wafalme 18 Tumuone Mtumishi wa Mungu alivyojega Madhabahu Yake Kwanza kabla hajamuita Mungu
Tunamuona hata ibrahimu Akajenga Madhabahu na akawa anatoa mafungu Yake ya kumi na kuendelea kumuona Mungu katika utoaji
Tunamuona Yoshua Akajenga Madhabahu akaweza kuwavusha watu kuingia kanani. Na wewe Unatakiwa Ujenge mahusiano yako Na Mungu Kwanza kabla hujaanza kuomba futa mahusiano yaliyombeba Shetani Kupitia uzinifu Kupitia wizi Kupitia kuacha kusali huendi kanisani
Karibuni wanangu
Naitwa Pastor Richard
Kanisa la Holy Spirit
Makao makuu
Morogoro veta Dakawa

Madhabahu siyo njego ni Agano LA MUNGU kwa mch. Wake Mtumishi wake ndani Yake yoyote mchungaji unayemuona anamadhabahu Yake yaani neema Yake ndani inayonena kwa Habari  ya kuwasaidia watu wenye matatizo na Shida sawasawa na Madhabahu Yake inavyonena ndani yake

✍🏾✍🏾 Madhabahu isiyo Yako Haiwezi Kukubadilisha kiroho au kimwili.

UKIONA HUJIBIWI MIAKA YOTE ujue

1:Madhabahu hiyo siyo Yako Yaani unapotoa sadaka Mafungu kusali sio kanisa au kwa Mch ambapo MUNGU ameandaa Majibu Yako.

2:UKIONA HUNA MABADILIKO YA KIMWILI na KIROHO ujue Madhabahu hiyo siyo yako Hapo unapozini sipo alipokuamdalia Majibu Yako MUNGU

3:UKIONA UNASUKUMWA KUWA LEO UMEENDA HUKU Kwenye maombi unaitafuta Madhabahu yako iliyobeba Majibu Yako  na utaipata tu Mch aliyebeba Majibu Yako

4:UKIONA UNATOA ZAKA YA FUNGU la kumi miaka mingi bila Kupokea Majibu Yako JUA hiyo siyo madhabahu yako

5:KILA MTU MAJIBU YAKE HUWA ILISHAANDALIWA UTAKAPOPONEA KWA HIYO UKIONA MWEZAKO Amejibiwa wewe hujibiwagi ujue hiyo madhabahu ya huyo Mch Haina Majibu yako

MAMBO YATAKAYO KUFANYA UJUE MADHABAHU YAKO

1:Utashuhudiwa Nenda kwa Mch fulani na utasikia msukumo hapa ndipo Majibu yangu yapo.

2:UTAPATA MUDA WA KUPAFIKIA NA MOYO WAKO ATAKUWA UNAAMANI YAKUPOKEA MAJIBU Yako

3:UTATOA FUNGU la kumi Utaona Mabadiliko katika maisha yako afya yako

4:UTABADILISHWA KIROHO NA KIMWILI UTAKUWA HUTORUDI nyuma

5:UTAOMBA HATA MWENYEWE UTAJIBIWA

6:HUTOVUNJIKA MOYO AU KUJIONA kama hutafuguliwa utakapochelewa kujibiwa

7:UTAFIKA KWA Mch atakueleza Matatizo yako yanasababishwa na nini na ufanyaje ili ujibiwe

8:UNAWEZA KUMUONA TU Mch Ukafunguliwa

. 9:Utakuwa kimaombi na kiimani

10:Mtafute MUNGU utafikia Madhabahu yako kadiri unavyohagaika Leo upo hapa Kesho pale unatafuta Madhabahu iliyo na Majibu Yako

✍🏾✍🏾Madhabahu iliyo yako lazima ikubadilishe kiroho kwa Muda tu. Na kimwili

✍🏾✍🏾Madhabahu isiyo yako lazima Izugumze juu ya matatizo ukiomba lazima ijibu

✍🏾✍🏾Madhabahu isiyo yako  haiwezi kujibu maombi yako hata usungue vipi magoti.

Ukiona umeomba umelia umetoa fungu la kumi  miaka mingi upo Hali ile ile kiroho Hakuna hatua ujue

Siyo mahali pako hapo MUNGU alipokuandalia au kukuweka  yamkini umefata Baba mama kwakuwa walikuwa wakiabudu hapo nawe haipo hivyo Madhabahu hiyo

✍🏾Madhabahu huwa inakupokea kwa zaka Maombi utoaji Imani.

✍🏾✍🏾Kama wewe ukawa unaomba MUNGU NIPE Mme/NIPE mke Nipe hiki

Miaka yote haijibu zaka unatoa zaka unatoa hiyo Madhabahu haikujui Haikujui kabisa

SIRI ya Madhabahu huongea juu ya Mwenye Tatizo shida kupitia zaka fungu LA kumi na Maombi tu nijibu

MUNGU huwa anakupa Au kukuletea Mchungaji Mwenye Madhabahu yako muda mchache utakapotoa zaka dhabihu sadaka

Kiroho utabadilishwa kimaombi nakujisimamia Mwenyewe utaweza

Utaweza kuomba na kuwa moto vizuri

Mengi utajibiwa kila uombalo utajibiwa

Utaomba utasikilizwa na utajibiwa

Maana MUNGU anasema Mimi nitakuongoza pa kukalisha na kunitolea Mimi fungu LA kumi nitasema na moyo wako nitasema nawe🎤🎤kumbukumbu. Torati.14;22-26

MUNGU hutuondoa katika Madhabahu isiyozugumuza juu yetu kwa kutupa wachungaji wengine imladi tu Aweze kukubariki

Ni lazima utoke katika  Madhabahu ambayo haikutambui uingie Madhabahu inayokujua ili ukabarikiwe ili maisha yako yakabadilishwe Yakawe Kama ilivyoahidiwa

Madhabahu yako Utaijuaje

1:Hukubadilisha kiroho unakuwa sio miaka yote unanyonyeshwa hukui

2;Hukupandisha katika viwango vya kiroho Maombi unakuwa mzuri.

3;Hukufanya usimame mwenyewe

4;Hukujibu ukiomba katika Mafungu ya kumi

5;Hukubariki

🎤🎤Somo hili chunguza Madhabahu yako Kama inajibu tulia Nayo hiyo ndio yako kama haikujibu Muombee Roho Mtakatifu akupe Mahali Pako

Hapo hapo Utamtolea Fungu LA kumi

Sadaka

Utahudhuria Utaratibu WA masomo

Utaendeleza Maombi ukiwa hapo atakapokuweka Bwana au mlezi atakayekupa msikilize Mlezi wako wa kiroho

Madhabahu ukizichanganya changanya huwa hazijibu Wala kukupa matokeo

Tulia pale unapowekwa ili Madhabahu iseme nawe upokee majibu yako

🎤🎤Nimewaandikia Walaka huu ili msiwe mnalaumu wachungaji au kanisa hapana ukiona hujibiwi ni Madhabahu  Tu

Madhabahu ikiwa haikujui mpaka unazeeka humo hujawahi kubarikiwa imladi tu unaemda kanisani lakini wezako wananunua magari wewe Mpaka uende kwa wenyeji

Wakati huo wezako Fungu LA kumi linabadilisha maisha yao lakini wewe ipo tofauti

Soma mwanzo.12 yote

🔚By Pastor Richard

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

NDOTO 20 ZA SHULENI TU MAZINGIRA Ya SHULE

SOMO: NGUVU YA KUJITAMBUA

SOMO:ADUI NA JINSI YA KUMKABILI ADUI YAKO.