MISTARI ya KUSOMA USIKU WA MANANE Katika MAOMBI
MISTARI YA KUSOMA USIKU HUU TUNAPOINGIA MAOMBI YA USIKU WA MANANE TUNAANZA SAA SITA USIKU MPAKA SAA KUMI ALFAJIRI KILA SIKU. Group:MAOMBI NA MAFUNDISHO Admin;Pastor Richard. WhatsApp Kujiunga+255710889892 Yeremia 33:3 Niite, nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua. Kutoka 34:13 Bali utabomoa madhabahu zao, na kuvunja-vunja nguzo zao, na kuyakata-kata maashera yao. Kutoka 14:14 Bwana atawapigania ninyi, nanyi mtanyamaza kimya. 2 Wakorintho 10:4 (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;) Kumbukumbu la Torati 28:7 Bwana atawafanya adui zako wainukao juu yako kupigwa mbele yako; watakutokea kwa njia moja, lakini watakimbia mbele yako kwa njia Saba. ...