MAOMBI YA USIKU WA MANANE 2026/3/4
Group: MAOMBI NA MAFUNDISHO Admin Pastor Richard Wa Morogoro WhatsApp group Jiunge+255710889892 HATUA ZA KUOMBA USIKU HUU WA MANANE Mwal:Pastor Richard Nipo Morogoro Veta Dakawa Kanisa la Holy Spirit Maandalizi ya Kiroho ππΎππΎππΎππΎ Kabla ya kuanza, hakikisha umetubu na kusafisha moyo wako. Waefeso 6:12 inatukumbusha kuwa vita vyetu si juu ya damu na nyama, bali ni juu ya falme na mamlaka. π₯ Maombi ya Vita vya Kiroho 1. Kujifunika kwa Damu ya Yesu "Baba katika jina la Yesu Kristo, naja mbele zako usiku wa leo. Ninajifunika mimi, nyumba yangu, na familia yangu kwa Damu ya Yesu. Ninachora mstari wa moto kuzunguka mipaka yangu; adui asipate nafasi ya kupita. Damu ya Yesu iwe kinga na ukombozi wangu usiku huu wote." 2. Kubomoa Mitego ya Adui "Ee Bwana, kila mtego uliotegwa na adui gizani kwa ajili ya usiku wangu, ninaung'oa kwa jina la Yesu! Kila kikao cha wachawi, waganga, au mamlaka za giza kinachopangwa dhidi yangu, kikasambaratike kwa Moto wa Roho Mtakat...