SOMO WANANDOA MPATANE
DARASA LA WANANDOA SOMO👉🏿 WANANDOA MNATAKIWA KUPATANA. Mathayo:20:13 Marko:14;56 Mithali:9;9 KUPATANA Ni Kuelewana kwa Wanandoa Ili muweze kuishi vizuri ndani ya ndoa huwa MNATAKIWA mpatane Kwa haya Naitwa Pastor Richard Mwalimu wa Wanandoa Somo Hili linahusu miaka 18-60 1:KUPATANA KWA MIPANGO YENU Mipango Ni mikakati yenye Kuleta Maendeleo na kuifanya ndoa Yenu Iwe na Msingi mzuri wa Maendeleo nakuinuka Kiuchumi. 2: KUPATANA KWA MATUMIZI YA PESA Wanandoa MNATAKIWA mpatane katika matumizi ya Pesa nakudhibiti matumizi yasiyo ya lazima kuweka bajeti Yenu Na Kupangilia Nini mfanye Nini msifanye kwa muda huo. 3: KUPATANA KWA UZAZI. Mnatakiwa Wanandoa mzae Watoto mtakaoweza Kuwalea nakuwatuza Vizuri msizae tu Watoto bila mpagilio au kuangalia Uwezo wa kuwasomesha na kuwatunza 4:KUPATANA KWA IMANI. Wanandoa MNATAKIWA mpatane maswala ya imani kila mmoja awe huru kuweka wazi kadiri Im...