SOMO:VIFO VYA MITUME WA KRISTO
SOMO:JINSI MITUME WALIVYOKUFA. Naitwa Pastor Richard Nakukaribisha Ujifunze Vifo vya mitume wa Yesu/ jinsi mitume walivyokufa. Itakujenga imani Mtume pekee ambaye biblia inarekodi mauaji yake jinsi yalivyokuwa ni mtume Yakobo ndugu yake mtume Yohana. Huyu biblia inasema katika Matendo 12:1-2, kuwa Mfalme Herode alimuua kwa Upanga, alikatwa kichwa. Lakini kwa habari ya mitume wengine waliosalia biblia haijarekodi jambo lolote kuhusu vifo vyao. Hivyo ili kupata taarifa zihusuzo huduma zao na vifo vyao ilipasa watu warejee katika hadithi ambazo zinaamika ziliandikwa na watu ambao walikuwa karibu sana na mitume, au walioshuhudia vifo vyao. Japo habari hizo hatuwezi kuzithibitisha kuwa zina usahihi wa asilimia mia, lakini kwa sehemu kubwa zimethitishwa kuwa kweli, kulingana na kupatana kwa maneno ya mashuhuda. Mathayo: Mathayo alijeruhiwa vibaya na upanga alipokuwa anahubiri katika nchi ya Ethiopia kaskazini mwa Afrika. Na baadaye kukumbwa na mauti kuto...