SOMO ZIJUE SIKU ZA KUPATA MIMBA
*SOMO:NJISI YA KUELEWA SIKU ZA KUPATA MIMBA* Na Sababu zinazofanya Wanandoa wasizaye haraka kutokujua Elimu hii Ufunuo:12:2 Isaya 26:17 Ayubu:3:3 YAI KUPEVUKA HUA HATUA YA KWANZA KUIJU Yai la Mwanamke hupevuka siku 14 kabla ya ya siku ya bleed. Hii ni siku muhimu sana kwa wana ndoa kuijua. Siku hii yai huwa linakuwa limeshakomaa na tayari limeshatoka katika nyumba yake ya mayai (ovaries) na kuelekea katika mirija ya uzazi (fallopian tube) tayari kukutana na mbegu ya kiume. Na kumbuka mbegu za kiume huishi muda wa masaa angalau 72 kwa hiyo muda wowote ndani ya masaa 72 kabla ya yai kutoka katika ovaries mtwanamke anaweza kudungwa mimba. Mfano kama yai linatoka tarehe 13, basi ukifanya tenbdo la ndoa siku ya tarehe 13,12,11,10 zote unaweza pata mimba - kwa hiyo hizi huitwa siku za mimba (fertile days), tofautisha na siku za hatari ambazo ni kuanzia siku yai limetoka na siku kadhaa baada ya yai kutoka.  *KWA NINI BAADHI YA WANANDOA HUCHELEWA KUTUNGA MIMBA* ? Kupata mtoto...