SOMO:HATUA ZA MSINGI ZA KUKUA KIROHO
SOMO: HATUA ZA MSINGI KWA MWOKOVU MPYA (KUKUA NA KUDUMU KWENYE WOKOVU) Kuokoka ni kama kuzaliwa mara ya pili. Mtoto mchanga anahitaji maziwa, matunzo, na ulinzi ili akue na kuwa mtu mzima. Vivyo hivyo, mwokovu mchanga anahitaji mambo yafuatayo ili asirudi nyuma: Karibuni Ufatane Nami Naitwa Pastor Richard Wa Morogoro WhatsApp+255710889892 Mbarikiwe Wachungaji Mnaochukuaga Masomo haya nakuwafundishia Waumini Kanisani ili Kulikunza Na Kuliimarisha Kanisa. 1. Neno la Mungu (Chakula cha Kiroho) Kama vile mwili unavyohitaji chakula, roho inahitaji Neno la Mungu ili ipate nguvu na maarifa. Unatakiwa upate Mafundisho ukiokoka Tu Hakikisha Unahuzuria Mafundisho Yatakayokujengea Msingi Wa Kuimarika Kiroho weka ratiba ya Kusoma Biblia Cha kufanya: Anza kusoma Biblia kila siku. Inashauriwa kuanza na Injili ya Yohana ili kumjua Yesu vizuri. Mstari: "Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili kwa hayo mpate kuukulia wokovu." ( 1 P...