Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili 23, 2026

SOMO; NGUVU YA UMILIKI WA UKOO

SOMO: NGUVU YA UMILIKI KATIKA UKOO Naitwa Pastor Richard Wa Morogoro Katika Familia au ukoo huwa Lazima Uwe na Nguvu ya kumiliki. Mfano: Elimu madaraka Imani na Pesa Familia Yoyote Lazima Awepo Mtu mwenye cheo kama familia Ya Yese Au Ibrahimu nk ​Neno Kuu: “Mtu mwema huwaachia wana wa wanawe urithi; na mali ya mwenye dhambi huwekewa mwenye haki.” (Mithali 13:22) ​1. Msingi wa Umiliki: Agizo la Kiungu ​Mungu ndiye aliyeanzisha mfumo wa koo na familia, na alikusudia kila ukoo uwe na sehemu yake ya kumiliki ili kujiendesha. ​Andiko:  Mwanzo 1:28   "Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha..." ​Tafakari: Kuitiisha nchi maana yake ni kuitawala na kuimiliki. Ukoo usioiliki rasilimali hauwezi "kuitiisha" nchi, badala yake unatiishwa na kutaabika. ​2. Umiliki wa Ardhi na Urithi wa Kudumu ​Katika Biblia, ardhi haikuwa mali ya mtu mmoja tu, bali ilikuwa ni dhamana kwa ajili ya ukoo mzima ili kuhakikisha hakuna kizazi kinachokuja ku...