Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Mei 4, 2026

SOMO; MBINU ZA KUVUNA WATU

SOMO: MBINU ZA KUVUNA WATU NA KUWALETA KWA YESU Karibuni SOMO hili Nzuri ​Kuvuna watu (Uinjilisti) si kazi ya wahubiri pekee, bali ni agizo la kila mwamini. Ili kufanikisha hili, tunahitaji mkakati wa kiroho na wa kiutendaji.Naitwa Pastor Richard Nipo Morogoro Karibu.  ​1. Maandalizi ya Kiroho (Maombi ya Upatanisho) ​Kabla ya kusema na watu kuhusu Mungu, lazima useme na Mungu kuhusu hao watu. Maombi hulegeza mioyo migumu na kufungua milango ya ufahamu. ​Andiko la Kusoma:- : “Basi, kabla ya mambo yote, nataka dua, na sala, na maombezi, na shukrani, zifanyike kwa ajili ya watu wote.” (1 Timotheo 2:1) ​Mambo Ya Kufanya: 1:​Omba Roho Mtakatifu akupe 2: "Macho ya Kiroho" kuwaona wenye uhitaji..  ​3:Vunja ngome za shetani zinazowazui 4:​Omba Mungu akukutanishe na mtu ambaye moyo wake umeshaandaliwa. ​2. Jenga Uhusiano wa Upendo (Ushuhuda wa Maisha) ​Watu wengi huvutiwa na tabia yako kabla hawajavutiwa na maneno yako. Upendo ni lugha inayoeleweka na kila mtu. ​Andiko la Kusoma “Vivy...