Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili 15, 2026

SOMO:WANAWAKE WANAOSALITIWA HUWA KUNDI HILI LIJUE

​SOMO:WANAWAKE WANAOSALITIWA HUWA KUNDI HILI  LIJUE.  Rejea Vitabu:Mithali;8;10 Mithali;12;1-5 Karibu Sana Mwana NDOA  Katika DARASA Hili Uongeze Ufahamu Wa Kujifunza ili Uwe na Ufahamu usiendelee Kulizwa Kwenye Mahusiano Karibuni Tuwe Pamoja.  Naitwa Pastor Richard Wa Morogoro WhatsApp+255710889892 1. Wanawake "Wanaojitolea Kupitiliza" (The Over-Givers) ​Hawa ni wanawake ambao huweka kila kitu chao kwa mwanaume—fedha, muda, na hisia—huku wakisahau mahitaji yao wenyewe. ​ Sababu ya kuumizwa:   Mwanaume anaweza kuanza kumchukulia mwanamke huyu kama "shamba la bibi" au sehemu ya samani (taken for granted), na hivyo kukosa hofu ya kumpoteza kwa sababu anajua atakuwepo daima hata akifanya makosa. ​2. Wanawake Wanaovumilia "Vichocheo vya Hatari" (Red Flags) ​Kundi hili huona dalili za usaliti au tabia mbaya mapema lakini huchagua kuzipuuza kwa matumaini kuwa mwanaume atabadilika. ​ Sababu ya kuumizwa:   Huamini kuwa upendo wao una nguvu ya "kumtibu" a...

SOMO:NGUVU YA KUTAFSIRI UNACHOKISIKIA

SOMO: NGUVU YA KUTAFSIRI UNACHOKISIKIA.  ​Utangulizi: ​Kusikia ni tendo la kibiolojia (masikio kupokea sauti), lakini Kutafsiri ni tendo la kiakili na kiroho (kutoa maana). Nguvu ya maisha yako haitegemei kile unachokisikia, bali inategemea tafsiri unayoipa sauti hiyo. MASIKIO HUSIKIA:Kinachoongelewa AKILI HUTOA TAFSIRI:Hutoa Maana Ya Kile ulichosikia.  .  Watu Wengi Wanakosana Kwenye Eneo la Kusikia Lakini Akili inakuja kutafisiri makosa au Vibaya nakijenga chuki Kati ya Mtu na Mtu au kundi na Kundi.  Naitwa Pastor Richard Wa Morogoro WhatsApp+255710889892 Maandiko na Misingi ya Somo 1. Nehemia 8:8 "Nao wakasoma katika kitabu, katika sheria ya Mungu, kwa sauti ya kueleweka; wakatoa maana yake, hata wakayaelewa yale yaliyosomwa." • Fundisho: Nguvu haipo kwenye kusoma au kusikia tu, bali kwenye kutoa maana (tafsiri) inayopelekea uelewa. 2. 1 Wakorintho 14:13 "Kwa sababu hiyo yeye anenaye kwa lugha na aombe ili apate kuitafsiri." • Fundisho: Mawasiliano yasiyo na tafs...