SOMO;MAOMBI 46 YA KUMTEKETEZA SHETANI

SOMO;MAOMBI YA KUMTEKETEZA SHETANI:
NA NGUVU ZAKA
Vitabu vya Kusimamia Tusome
2Wakoritho;10;3-6 Maombolezo;3;33 Yeremia;29;11-14

Omba rudiarudia mara 5 kila ombi
Muda tulivu ndio uombe
Naitwa Pastor Richard 
WhatsApp +255759861768

1. Ninayaharibu na kuyateketeza mamlaka yote aliyopewa shetani na mababu/ mababa, ndugu zangu katika Jina la Yesu.
2. Nina zilaani na kuziteketeza kwa damu ya Yesu roho zote zinazoendelea kutilia mkazo hayo maagano katika maisha yangu na naziteketeza na kuzivunavunja kwa Jina la Yesu.
3. Kitu chochote kilichoingizwa kwenye maisha yangu,kwa mkono wa kipepo, au majini ninakiamuru kiachie kwa JIna la Yesu.
4. Kila aina ya sumu iliyopenyezwa kwenye maisha yangu nina iamuru itoke nje sasa, katika jina la Yesu, nina sukuma nje kwa damu ya Yesu.
5. Ee Bwana Yesu, shusha moto juu ya kila roho ya mauti na kuzimu, iliyoandaliwa kwa ajili yangu, katika jina la Yesu
6. Nina ponda kichwa na kukanyaga kila mkia wa majoka ya kiroho, katika jina la Yesu
7. Upanga wa moto, na uanze kukata kila kifungo walichokifunga wazazi, katika jina la Yesu
8. Ee Bwana, nifunulie agano lolote la siri ambalo shetani amefunga na nafsi yangu au anataka kufunga na nafsi yangu, katika jina la Yesu.
9. Kila pando,ambalo baba yangu wa mbinguni hakulipanda katika maisha yangu, nina kungo’a katika jina la Yesu.

10. Baba nina pitisha umeme katika ardhi ya mahali hapa sasa na kila agano na miguu yangu lianze kuvunjika sasa katika jina la Yesu.
11. Agano lolote la siri ambalo ni la uovu, ninakuvunja katika jina la Yesu
12. Nina nyunyiza damu ya Yesu kuvunja laana zote
13. [Imba wimbo huu kama unaweza, kama huwezi usilazimshe: Kuna nguvu ya ajabu, damuni mwa Yesu ]
14. Nina nyunyiza damu ya Yesu kuvunja laana zote za dhambi za wazazi wangu
15. Ee Bwana, badili laana zote zilizoelekezwa kwangu kuwa Baraka
16. Kila nguvu ya uovu iliyoelekezwa kwangu, ninakuamuru kurudi moja kwa moja, kwa mtumaji katika jina la Yesu.
17. Ee Bwana Mungu, ninaomba kila alichosema adui kwamba hakitawezekana katika maisha yangu, kikawezekane sasa kwa jina la Yesu.
18. Nina jiondoa na kujitenganisha katika kambi yoyote ya mateka inayomilikiwa na adui,katika jina la Yesu.
19. Nina jifungua na kujiondoa kutoka kwenye kila kifungo cha kurithi ,katika jina la Yesu.
20. Ee Bwana,tuma shoka lako la moto kwenye misingi ya maisha yangu na uharibu/ulikate kila pando ambalo amelipanda adui katika jina la Yesu.
21. Nina ipitisha Damu ya Yesu, katika mifumo yote ya mwili wangu [mfumo wa damu, wa fahamu, wa chakula, wa upumuaji, wa takamwili n.k] na kuisafisha mabaki yote ya urithi wa vitu viovu katika jina la Yesu.
22. Damu ya Yesu na moto wa Roho mtakatifu,unisafishe kila kiungo cha mwili wangu [Figo, moyo, mapafu, macho, masikio, n.k] katika jina la Yesu
23. Nina vunja mikataba yote ya kiukoo na kikabila inayonihusisha mimi katika jina la Yesu.
24. Nina jiondo/ninajivua/vunja laana zote za kikabila na kiukoo katika jina la Yesu
25. Nina tapika chakula chochote cha uovu nilicholishwa katika maisha yangu, katika jina la Yesu
26. Mapepo, majini, mizimu na wachawi manao fuatilia maisha yangu,na mpararaizi[mpooze] sasa katika jina la Yesu.
27. Shambulio lolote lilopangwa juu ya familia yangu, ninalibatilisha kwa ajili yangu katika jina la Yesu
28. Nina vunja matoke mabaya yote kwa ajili ya jina la kiuovu, lilipachikwa kwenye nafsi yangu katika jina la Yesu
29. Nina batilisha laana zote, mikosi, majanga, ajali, maradhi yote yaliyoelekezwa kwenye maisha yangu katika jina la Yesu.
30. Muombe Mungu aondoe laana zote alizo ziachilia kwenye maisha yako kwa sababu ya kutotii neon lake[kumb 28:]
31. Pepo lolote lililo jipachika kwenye laana yoyote inayonihusu mimi, toka, katika jina la Yesu
32. Laana zote katika maisha yangu, badilika na kuwa Baraka, katika jina la Yesu
33. Utakapokuwa unataja laana zilizoorodheshwa hapo chini, sema kwa kumaanisha “vunjika, vunjika, vunjika” katika jina la Yesu. Nina jitenganisha na nyinyi katika jina la Yesu.
• Laana zote za udhaifu wa kiakili na kimwili
• Laana zote za kushidwa katika kila ninalofanya
• Laana zote za umaskini
• Laana zote za kuvunjika kwa familia
• Laana zote za kuonewa na kudharauliwa
• Laana zote za Uharibifu wa mtu binafsi,kama vile kujinyonga n.k
• Laana zote za magonjwa sugu
• Laana zote za kishirikina
• Laana zote za kuharibikiwa mambo ya uzazi na viungo vya uzazi
• Laana zote za kufanya kazi kwa bidii pasipo kuiona faida
• Laana zote za kulowea mambo ya uovu kama vile zinaa, pombe, sigara n.k
34. Jitamkie maneno ya Baraka wewe mwenyewe, kwa mfano kwa kusema “hakutakuwa na umaskini tena, magonjwa tena n.k katika maisha yangu katika jina la Yesu.
35. Nina jifungua na kujitenganisha na vifungo vya madhabahu zote za giza katika jina la Yesu.Sema mara kadhaa ukifuatiwa na maneno yafuatayo “nina jitenganisha” katika jina la Yesu.Tumia muda kidogo kwenye hilo.
36. Nina tapika sumu zote za mashetani nilizozimeza katika jina la Yesu.
37.[Weka mikono yako juu ya kichwa chako] Nina vunja kila mamlaka za giza katika maisha yangu, katika jina la Yesu.Rudia “nina vunja katika jina la Yesu.
38. Taja mambo yafuatayo kwa mamlaka na sema “vunjika kwa jina la Yesu.
• Mamlaka zote za mizimu na miungu ya familia, ukoo, na kabila
• Mamlaka zote za roho za kichawi zilzopo ndani ya familia, ukoo, kabila
• Mamalaka zote zilizoshika rimoti za kudhibiti familia, ukoo, kabila
• Mamlaka zote ovu ndani ya Familia, ukoo, kabila nk
39. Kila mmiliki wa mzigo niliobebeshwa beba mzigo wako katika jina la Yesu[Mzigo unaweza kuwa ugonjwa,mikosi wabebeshe wamilki]
40. Nina zipoodhesha/nina zipararaizi madhabahu zote za giza katika jina la Yesu
41. Nina zilaani madhabahu zote za uovu zilizoelekezwa zidi yangu katika jina la Yesu
42. Nina agiza nyundo ya Mungu aliyeumba mbingu na nchi,iponde kila madhabahu ya giza zilizoelekezwa kwenye maisha yangu katika jina la Yesu.
43. Ee Bwana tuma moto wako na uteketeze madhabahu zote za giza zinazoinuka dhidi ya maisha yangu,
44. Makuhani wote wa madhabahu zote za giza wanaocheza na maisha yangu,wakutane na upanga wa roho mtakatifu. Katika jina la Yesu.
45. Mkono wowote unaotaka kunikamata na kuniteka kwa ajili ya Maombi haya ninayoomba kauka katika jina la Yesu.
46. Nina waamuru makuhani wa madhabahu za giza kunyweni damu wenyewe katika jina la Yesu

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

NDOTO 20 ZA SHULENI TU MAZINGIRA Ya SHULE

SOMO: NGUVU YA KUJITAMBUA

SOMO:ADUI NA JINSI YA KUMKABILI ADUI YAKO.