SOMO: Tofautisha mwanamke na mschana

✍️✍️SOMO; UNAJUA UTOFAUTI YA WANAWAKE NA WASCHANA KATIKA MAHUSIANO

✍️✍️Darasa la Wanandoa
✍️✍️Mwal; Pastor Richard
✍️✍️SIMU +255759861768

Mithali;14;1 Waefeso;5;22 Mithali;7;7

✍️✍️✍️Tunakutana Tena Katika Darasa la Wanandoa Tunapoongelea Mwanamke Ni Bint AMBAYE Ufahamu wake Anajua Maana maisha ya Ndoa na maana kuitwa MKE Ndani ya ndoa.

MSICHANA Ni Bint Ambaye Bado hajui maana ya ndoa au Maumivu katika mahusiano hajui Wala haelewi wanaume wanatofautiana

Karibu Uwaone WASCHANA Kwanini humizwa na Wanawake hawaumizwi

1. Wasichana wanatafuta wanaume wenye pesa ila Wanawake wanatafuta wanaume wanaojali na kupenda.

2. Wasichana hupima thamani ya wanaume wao kwa kuangalia ukubwa wa mifuko yao ila Wanawake hupima thamani ya wanaume wao kwa kuangalia kiwango cha busara na hofu ya mungu na kwa vipi wanajiheshimu mbele ya wapenzi wao.

3. Wasichana huvunja mahusiano kwa sabubu zisizo na mashiko ila Wanawake wana uvumilivu wakifahamu kwamba kila jambo hutokea kwa sababu.

4. Wasichana hufikilia kuhusu mambo yaliyopo sasa ila Wanawake hufikilia kuhusu yajayo.

5. Wasichana wanapenda kuwa na wanaume wengi wanaowafuata ila Wanawake wanafahamu sheria ya uhitaji (Vitu rahisi vina wateja wengi).

6. Wasichana wanahitaji pesa ili kununua make-ups ila Wanawake wanahitaji pesa kwa ajili ya kufanyia mipango ya maendeleo.

7. Wasichana huumizwa na mwanaume mmoja na kuwa na kinyongo na wanaume wote ila Wanawake wanajua kwamba wanaume wote sio sawa.

8. Msichana "anajifunza" ila Mwanamke "anajua"

Naitwa Pastor Richard

Comment na Share  Masomo haya.✍️🙏

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

NDOTO 20 ZA SHULENI TU MAZINGIRA Ya SHULE

SOMO: NGUVU YA KUJITAMBUA

SOMO:ADUI NA JINSI YA KUMKABILI ADUI YAKO.