SOMO:ISHARA ZA PAKA KIROHO ZILIZOHATARI
SOMO: ISHARA ZA KIROHO ZA PAKA NA USHINDI DHIDI YA MAAGANO YA GIZA
Mwalimu: Pastor Richard (Morogoro)
UTANGULIZI
Ulimwengu wa roho hauna midomo ya nyama, hivyo hutumia ishara na viumbe hai kufikisha ujumbe au mashambulizi. Paka amekuwa akitumiwa kwa karne nyingi kama chombo cha upelelezi na madhabahu za kichawi. Muumini anapaswa kuwa na macho ya rohoni ili kutofautisha kati ya paka wa kimaumbile na paka aliyetumwa kama wakala wa giza.
Ninaitwa Pastor Richard Wa Morogoro Veta Dakawa WhatsApp+255710889892
Hurusiwi kufuta au kuongeza hili ni somo la Kiroho soma mwisho naelekeza namn
Mstari wa Msingi Tunaosimamia
"Mwe na kiasi, kesheni; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ameze." (1 Petro 5:8)
SEHEMU YA KWANZA: ✍🏾ISHARA 7 ZA KIROHO ZA PAKA
1. 1⃣➖PAKA KULIA SAUTI KAMA MTOTO NJE YA NYUMBA YAKO
Paka wanapogombana wakilia kama watoto wachanga, ni ishara ya vita dhidi ya Hatima (Destiny). Wanapigania nyota yako au ya watoto wako ili kuizima kabla ya wakati au kuharibu kabisa maisha Yako Jitaidi kemea Hiyo Ishara SEMA Mipango Yenu Imeshindwa Kwa Jina la Yesu.
Mstari Wa Kusoma ni huu;-
- : Mathayo 2:16 (Mashambulizi dhidi ya watoto/maono mapya).
2. PAKA KUPIGANA KWENYE MLANGO AU UKUTA WA NYUMBA UNAPOISHI.
Huu ni uvamizi wa malango ya nyumba yako. Wanajaribu kujenga madhabahu ya kuzuia baraka zisiingie na kuruhusu mikosi na balaa kupenya ndani. Utaanza kuona mikosi na kugombana ndani Ya nyumba au familia Yako. Kemea hii Hali Useme Ninakata na kuribu Madhabahu zenu Katika Jina la Yesu. Ameen
Mstari Wa Kusimamia
- Zaburi 24:7 (Vita vya malango)
- .
3. PAKA KUPIGANA JUU YA PAA
Paa inawakilisha ulinzi (Covering).
Paka wanapopigana juu ya paa, wanaachilia roho ya mafarakano, kelele, na kutokuelewana kati ya mume, mke, na watoto Ukiona Ishara hii kemea
Mstari Wa Kusimamia
- Mathayo 12:25 (Nyumba iliyofitinika).
4. PAKA KUPITA KATIKATI MLIPOKAA AU KUSIMAMA
Paka anapopita kwa kusisitiza katikati ya watu wawili wanapoongea jambo la heri, ni ishara ya roho ya fitina na utengano wa kimaagano. Omba kukemea Hapatakuwa na roho ya mafarakano na kemea Katika Jina la Yesu.
MSTARI WA KUSIMAMIA:
- Mithali 6:19 (Wapandao mbegu za fitina).
5. PAKA KUPANDA KITANDANI ANALALA NA WEWE AU ANAKAA KWENYE KITI ULIPOKAA
Paka wa ajabu kuingia ndani na kulala sehemu yako ya mapumziko ni ishara ya upelelezi wa kiroho na kupanda mbegu za uchovu au magonjwa ukiwa umelala. OMBA Kukemea Hiyo Hali na mfukuze atoke
Mstari Wa Kusimamia;-
- Mathayo 13:25 (Adui kupanda magugu usiku).
6. PAKA KUKUTAZAMA MACHO BILA WOGA.
Paka kukutazama machoni bila kupepesa kwa muda mrefu ni jaribio la adui kupandikiza roho ya hofu na kuiba ujasiri wako wa kiroho. Omba Kila ujasiri na Imani Yangu Haitaibiwa Kwa Jina La Yesu. Amen
Mstari Wa Kusimamia:-
- : 2 Timotheo 1:7 (Mungu hakutupa roho ya uoga).
7. PAKA KULETA PANYA AU CHOCHOTE ALICHOKIUA MLANGONI PAKO
Paka kuleta panya au ndege mfu na kumuacha mlangoni pako ni( "Sadaka ya madhabahu") inayolenga kunasa hatima yako unapovuka au kuigusa.hii huwa unapogusa chochote kilichokufa mlagoni bila Kukemea unajiugamanisha Katika mateso
Mstari Wa Kusimamia:-
- : Isaya 54:17 (Silaha zinazofanywa juu yako).
SEHEMU YA PILI: NINI CHA KUFANYA (MWONGOZO WA USHINDI)
- ➖1⃣:Kutumia Mamlaka ya Sauti:✍🏾.
- Usikae kimya. Kemea kwa sauti kwa jina la Yesu. Amuru kila wakala wa giza aondoke katika mazingira yako.
- Mamlaka: Luka 10:19 – "Nimewapa mamlaka ya kukanyaga nyoka na nge... wala hakuna kitu kitakachowadhuru."
-
- ➖2⃣:Kuvunja Maagano na Alama: ✍🏾Ikiwa kuna kitu kimeachwa mlangoni (mzoga), usikishike kwa mikono mitupu.
- ➖3⃣:Kutakasa Mazingira:
- ✍🏾Chukua maji na mafuta yaombee Hivi;
- Haya mafuta nayabariki Yawe nguzo ya Moto nguzo ya Nuru Nguzo ya Ulizi Kuta za nyumba Yangu Nazimiliki Katika Jina Yesu. ameen
- ➖4⃣:MAOMBI Ya USIKU WA MANANE
- ➖5:Kuimarisha Ulinzi wa Ndani:
- ✍🏾 Hakikisha maisha yako ni masafi mbele za Mungu. Adui hapati nafasi mahali ambapo nuru ya Kristo inatawala.
- Hakikisha Unasimama Imara na Mungu
- Yohana 14:30 – "...maana yuaja mkuu wa ulimwengu huu, wala hana kitu kwangu."
HITIMISHO:
Muumini aliyeokoka ana nguvu zaidi ya kiumbe chochote kilichotumwa na kuzimu. Ishara hizi zisiwe sababu ya hofu, bali ziwe kichocheo cha kuongeza umakini katika maombi na ulinzi wa mazingira yako
Maoni
Chapisha Maoni