Ruka hadi kwenye maudhui makuu

SOMO:MAOMBI YA UKOMBOZI WA NYOTA

SOMO ;MAOMBI YA UKOMBOZI WA NYOTA YAKO 

UTANGULIZI :
Karibu Naitwa Pastor Richard Nipo Morogoro Veta Dakawa  Tulia usome kisha tuombe wote tukomboe nyota zetu.
Fatana nami katika  Somo hili Ujifunze uelewe nyota kibiblia. Kila mtu huwa amezaliwa na nyota yake kabisa isipokuwa katika kuishi watu wengi hujichanganya kwenda kwa waganga na kuanza kushiriki vitu vya kiganga au kuchanjwa chali kama watoto hawakufanya wazazi inawezekana walienda kwa waganga.

NYOTA; huchukuliwa katika mazingira yafatayo 
-Kwenda kwa waganga 
-Kuishi maisha yakuzini unatubu unaridia kuzini
-Dhambi ya uasi huharibu haraka nyota yako

.UDHIBITISHO WA DHAMBI 

Mwanzo 3:9
[9]BWANA Mungu akamwita Adamu, akamwambia, Uko wapi? 
Dhambi ilisababisha uhusiano wa Adamu na Mungu kutoweka kuna kitu ndani ya Adamu kiliondoka. Nyota ya kuonekana ikapotea ndiyo maana Mungu anauliza upo wapi Adamu. 

MAANA YA NYOTA;

NYOTA: Ni utambulisho wa wewe ni nani katika maisha haya hatima yako ni ipi Kusundi lako ni nini kuwepo ..?

UDHIBITISHO WA ANDIKO;
Mathayo 2:2
[2]Yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana tuliiona nyota yake mashariki, nasi tumekuja kumsujudia. 

Yesu alipozaliwa watu walianza kumjua na Kumtambua ni mfalme kupitia nyota iliyomo ndani yake. Kuna utofauti mkubwa kuzaliwa kwa Yohana mbatizaji na Yesu.

Kumbe Tunajifunza Nini Adui hushughulika kuiwinda nyota yako ilimo ndani yako Apate kuiuwa isiwemo ndani yako mfano.
πŸ‘‰Kuuwa malengo yako
πŸ‘‰Kuuwa hatima yako
πŸ‘‰Kuuwa Kusundi lako na Mungu.

UDHIBITISHO WA HILI KWAMBA ADUI HUDILI NYOTA YAKO

Mathayo;2;7
[7]Kisha Herode akawaita wale mamajusi faraghani, akapata kwao hakika ya muda tangu ilipoonekana ile nyota. 

Adui Anapoona wewe unanyota ya mafanikio nyota kazi nyota ya ubunifu ataanza kukuwinda ili ahakikishe wewe hufanikiwi wewe hufikii hatua uliyokusundia ufike.
Mfano huyu mfalme Herode alitaka kuuwa malengo na kusundi la mtoto Yesu.

TUNAITAJI WAZAZI WA KIROHO WATAKAOTUKIMBIZA ADUI ASISHIKE NYOTA YETU.

Wazazi ni mhimu kwa maisha yako ya kiroho Tunaona Yusufu na mariamu kwa mtoto Yesu.
Mathayo 2:14-15

[14]Akaondoka akamchukua mtoto na mama yake usiku, akaenda zake Misri; 

[15]akakaa huko hata alipokufa Herode; ili litimie neno lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa nabii, akisema, 
Kutoka Misri nalimwita mwanangu. 

KAZI YA NYOTA NDANI YETU;

1:Nyota huleta Kibali.
Watu waliokosa kibali wapo wapo ni dhahiri nyota yao haionekani
TUSOMEπŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡
1samweli:2:26

2;NYOTA Hukupa Kazi.
Ukiwa na nyota kazi zitakufata mwenyewe kila unalofanya litaenda

 Mwanzo:41:13

Yusufu alikuwa mfungwa lakini kazi ilimfata huko huko gerezani hiyo ilikuwa ni nyota yake aliyonayo.

3;NYOTA HUKUPA UBUNIFU.

Waebrania;3;4

Hakika ukiona gorofa ujue kuna mtu kabuni ukiona Simu kuna mtu alibuni hicho ni kwa sababu ngani alianzisha nyota iliyomo ndani yake.

4:NYOTA HUKUPA MVUTO.

Waefeso:5:1

Utakuwa na mvuto kwa watu utapendwa sana na hautachukiwa hata ukisemwa vibaya utapata watu wanakutetea.


5;NYOTA HUMFANYA MTU ASIKILIZWE.

Yoshua;1;17

Yoshua alikuwa na nyota ya kusikilizwa na aliowaongoza na kuwasimamia.

6:NYOTA NDIYO HUKUPA MWELEKEO WA MAISHA YAKO YOTE.

Isamweli;17 hii hadithi inamzugumzia daudi jinsi maisha yake na mvuto wake aliokuwa nao kupitia nyota yake.


DALILI  ZA KUJUA NYOTA YAKO IMEIBIWA HAUNA NYOTA.

Kuna watu wanateseka hatima ya maisha yao hawaijui kutokana nyota haipo inatumiwa na watu wabaya kama wachawi ,waganga nk

1:UKIWA HUNA NYOTA UTACHUKIWA NA HAUTASIKILIZWA KWA MCHANGO WOWOT MKAAPO KIKAO CHA FAMILIA.

Mtu ukijiona familia yako au jamii haikusikilizi ujue nyota hiyo omba 


2;UTAKOSA MWELEKEO WA MAISHA YAKO.

Ukikosa mwelekeo hii hali hupelekea wegine kujiuwa wegine kuingia makundi mabaya mfano ujambazi vibaka au kujiuza.

3:UTAKOSA MVUTO.

Hutavutia kwa chochote hata ukiweka biashara hapo hutavuta mteja hata tu wakuuliza unachouza hutamuona.

Hali hii ukiona shughulika na maombi ya ukombozi wa nyota usichoke.


4:UNAKUWA KILA UNALOLIFANYA LINAKUWA CHINI YA KIWANGO ULICHOTAKA LIFIKIE.

Hali hii inayafanya maono yako yasiwe na nguvu sababu huna uwezo wa ufanisi wa unachokitenda.

5:MAMBO MENGI KUTOKUFANIKIWA.

Eneo moja unaweza tumia mamiaka mengi sana kutoka kwenda hatua nyigine unaweza ukashindwa kubadilika kumbe shinda ni nyota huna.


6;NYOTA UKIWA HUNA HATA NDOA Huwezi Kuwa nayo.


Haya ni niliyoeleza yakupe picha kutambua umhimu wa nyota yako ndani yako ili Tunapoingia maombi omba mpaka uone mabadiliko;


MAMBO YA KUZINGATIA UNAPOKUWA UNAIKOMBOA NYOTA YAKO.


1;Kama hujaokoka mpokee Yesu Awe mwokozi wako na akusaindie kuirejesha nyota yako.

SOMA HUU MSTARIπŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡

Yohana 1:12

[12]Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake; 

2:Anza Kutii na Kufanyia kazi Neno la Mungu 

SOMA MSTARI HUUπŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡πŸ‘‡

Kumbukumbu la Torati 28:1

[1]Itakuwa utakaposikia sauti ya BWANA, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo BWANA, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani; 

3;ANZA KUTOA FUNGU LA KUMI NA SADAKA 

Soma andiko

Malaki:3:8-14


MAOMBI TUNAVYOTAKIWA TUANZE.


OMBA TOBA KATIKA DHAMBI YA KUTOKUTII


"Baba Yangu wa mbiguni nisamehe dhambi ya kutokutii neno lako nilisoma neno ukaagiza niwe mwaminifu wa zaka na Sadaka lakini nimeshindwa kuwa mwaminifu katika kuomba umeniambia niombe lakinu mimi huwa siombi mimu huwa sifati maelekezo ya Mchungaji hata anaposema niombe namkubalia tu lakini sifanyi nisamehe Bwana nisamehe nitakuwa mtiifu kuanzia Leo Katika Jina la Yesu.Amen. 

Rudia ×2



KISHA INGIA MAOMBI YA KUIKOMBOA NYOTA YAKO. 

Maombi haya tembea tembea unaweza ukaabudu kwanza au kusifu kisha ukaanza kuomba tenga muda uliotulivu omba kwa hasira zote na mamlaka.


TUOMBE.


1:Baba katika Jina la Yesu ninavunja kila ukuta kila kibanzi mbele yangu kilichowekwa kuzuia nyota yangu isionekane Kwa Jina la Yesu Achia Kwa Jina la Yesu  Achia Achia navunja kila kizuizi kilichozuia nyota yangu isionekane katika Jina la Yesu.Amen 

Rudia ×4


2:Kamata Utosi unapoomba ombi hili la Pili.

"BABA Nakomboa utosi wangu nyota yangu katika milango yangu ya ufahamu ifuguke katika Jina la Yesu.Amen 

rudia rudia


3:Ombi la Tatu shikanisha mikono.

"Nakomboa uchumi wangu nyota yangu ya uchumi ikafunguke kila mikono ya umasikini ya kutokufanikiwa nasema itakasike ikaw na nguvu ya kushika uchumi kama ni Biashara nikiishika ifanikiwe katika Jina la Yesu.Amen 

Rudia ×3


4;OMBI LA NNE SAFISHA USO au kama paji la uso

"BABA Katika Jina la Yesu nafungua kibali changu cha kazi kibali changu cha ndoa kibali changu cha elimu kibali cha biashara kibali cha uzao kibali kwenda nje Katika Jina la Yesu Nyota yangu ikaangaze kwenye Kibali changu katika Jina la Yesu.Amen 

Rudia×3


5:Kamata Kila Panapouma Omba.

""Maumivu yote kila hali  inayoendelea kunishika kwenye viungo vyagu naamuru viniachie kila maumivu yaondoke katika Jina la Yesu.Amen

Rudia ×5


6:TUENDELEE OMBA KADIRI MSUKUMO WAKO NA MANENO YANAVYOKUJA TAMKA TAMKA NA TEMBEA TEMBEA USIKAE KAZANA MPAKA ROHO MTAKATIFU AMEACHA NAWE ACHA.





ndugu yangu maisha ya kiroho yaitaji uombe shughulikia kuikomboa nyota yako mwenyewe 


share maombi haya


namba za kuuliza kama hujaelewa nifate WhatsApp inbox +255759861768

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

NDOTO 20 ZA SHULENI TU MAZINGIRA Ya SHULE

SOMO: NGUVU YA KUJITAMBUA

SOMO:ADUI NA JINSI YA KUMKABILI ADUI YAKO.