SOMO;Hizi Sifa Za Mwanamke Mwema

SOMO:HIZI NDIYO SIFA ZA MWANAMKE MWENA NA MWENYE HOFU YA MUNGU 

Mwanzo;2;23-25 Mithali;14;1-5 Mithali;30;10

Ninaitwa Pastor Richard NINAKUKARIBISHA KATIKA ELIMU HII NA MASOMO YA WANANDOA NA MAHUSIANO  NATAKA NIONGELEE SIFA ZA MWANAMKE ANAEFAA KUOLEWA NA WAKUISHI NAE KATIKA MAISHA ATAKAEFANYA MAISHA YAKO YA FANIKIWE HII NI KWA VIJANA AMBAO HAWAJAOA 

KARIBUNI  FB; TAFUTA KANISA LA MOTO WA YESU UJIUGE

Kusamehe
Ni vigumu kuwa katika uhusiano halafu uwe hauna moyo wa kumsamehe mpenzi wako. Kawaida katika mahusiano, huwa kuna changamoto kadhaa ambazo hujitokeza hivyo lazima uwe na tabia ya kuweza kusamehe. Hii inaweza kuanzia kukosana kwa mambo ya kinyumbani, ama mambo mengine yanayofanana.

Mwanamke mzuri ni yule ambaye ana uwezo wa kumsamehe mpenzi wake bila kuweka kinyongo. Iwapo mpenzi wako umemshika katika fumanizi nk na bado unampenda, basi jambo zuri la kufanya ni kumsamehe na kuendelea na maisha.

Msikilizaji mzuri
Mara nyingi migogoro ambayo inatokea majumbani kati ya wapenzi wawili husababishwa na kutosikilizana. Huyu akiambiwa hivi huyu anajibu hivi. Iwapo mwanamke anataka mahusiano yake yake marefu na ya kufaana, basi anapaswa kuwa msikilizaji mzuri.

Mwanamke ambaye huwa anatulia na kumsikiliza mpenzi wake, mahusiano yake na mpenzi wake huwa ya furaha zaidi ukilinganisha na ya yule ambaye hatilii maanani maoni ya mwenzake.

Mwaminifu
Hii ni kuanzia kuongea ukweli bila kudanganya hadi maswala ya chumbani. Iwapo mwanamke ana mchepuko mahali fulani ama anamwendea kinyume mpenzi wake, basi aina hii ya tabia haifai kabisa.

Sifa ya mwanamke mzuri ni ile ambayo ni ya uaminifu. Mwanamke mwaminifu kwa mpenzi wake haitofika wakati fulani ambapo atakosana na mpenziwe.

Msaidizi
Katika mahusiano, kuna wakati fulani hufika ambapo lazima wapenzi wawili wasaidiane kufanya jambo ama kutimiza kitu fulani. Hivyo mwanamke mzuri ni yule ambaye anatoa msaada wa kumsaidia mpenzi wake na jambo fulani. Mathalan inaweza kuwa kumsaidia kimawazo, kifedha ama jambo tofauti. Mwanamke mwenye tabia hii humpendeza sana mpenzi wake kwa kuwa inaonyesha ya kuwa mwanamke kama huyu ana uwezo wa kumtumikia mpenzi wake wakati ambapo anaweza kupatwa na majanga.

Mwenye imani
Kuna tabia za wanawake ambazo huwachosha wanaume, nazo ni kukosa imani. Iwapo wewe una tabia za kutokuwa na imani basi tabia kama hio unafaa kuiacha mara moja. Tabia za kutokuwa na imani ni kama vile kuharakisha jambo, kulazimisha kitu ambacho hakiwezekani nk.

Hali kadhalika, mwanamke mwenye imani ni yule ambayo ana subira. Iwapo ameambiwa na mpenzi wake kuhusu jambo fulani, basi yeye hutulia hadi kungojea matokeo yake.

Kuhamasisha
Wanaume humpenda mwanamke ambaye anatoa motisha ili kumsaidia kutimiza lengo lake. Vile vile kwa kawaida kuna wanaume ambao wanahitaji kiinua mgongo ili kutimiza mambo fulani. Hivyo wewe kama mwanamke, mara moja au nyingine unafaa kuonyesha umotisha wako kwa kumuelekeza mpenzi wako mara moja au nyingine.

Mcha Mungu
Mwanamke mcha Mungu bila shaka maisha yake huwa ya kufanikiwa. Mtu yeyote yule lazima awe mcha Mungu ili awe na sifa nzuri ya maisha katika jamii.

Heshima
Heshima haimaanishi ni kwa mpenzi wako pekee bali kwa jamii nzima. Mwanamke ambaye anapenda kugombana na majirani kila kukicha halafu ikifika jioni anamheshimu mpenzi wake hafai.

Tabia za mwanamke mzuri ni yule ambaye anaheshimu na kuishi na majirani zake vizuri bila kuwa na mivurutano yeyote ile.

Anajiamini
Mwanamke mzuri ni yule anajiamini na anaamini mahusiano yake asiyekuwa na hofu kwa mme wake. Pale anaposikia Taarifa ya Tofauti kuhusu Mmewe humwita nakuongea nae.

ANAWEZA TENDO LA NDOA
Mwanamke mwema anajua Kuutumia mwili wake vizuri anapokuwa kwenye uwanja wa mahaba au kitandani Yeye Ni Zawadi nzuri ya mmewe mwanamke ukimkuta kwenye Tendo la ndoa hajui au Hapendi Kujifunza Kuhusu Ufanisi Mzuri wa Tendo la Ndoa au kujaribu mitindo Tofauti Tofauti. NDOA nyigi zinavunjika kutokana na Tendo la ndoa.


HITIMISHO 
TUFANYE NINI SASA TUWE MAKINI KATIKA KUAGALIA MTU WA KUOA KWA KUFATA SIFA HIZI

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

NDOTO 20 ZA SHULENI TU MAZINGIRA Ya SHULE

SOMO: NGUVU YA KUJITAMBUA

SOMO:ADUI NA JINSI YA KUMKABILI ADUI YAKO.