SOMO;THAMANI YA KIJANA NDANI YA KANISA.


SOMO: KIJANA THAMANI YAKE AKIOKOKA NDANI YA KANISA HATA KATIKA JAMII.


Karibu Tunaongelea Leo Thamani Ya Kijana mkristo Nafasi Yake kibiblia na mbele za Mungu. Kijana huandamwa na Tamaa mbalimbali na Changamoto za utafutaji Zinazomfanya Aishi mbali na Mungu Kutokana na Kuwa na muda mchache wa Kupumzika Mungu anatambua Kijana husumbuliwa na Tamaa za Pesa Mali Ujana Ukisoma 2Timotheo:2:22


Karibu Katika Darasa Hili Naitwa Bishop Richard

Nipo Morogoro Veta Dakawa



MAMBO SABA YA MSINGI YA KUKUSAIDIA KUTAMBUA THAMANI NA NAFASI YAKO KAMA KIJANA MKRISTO

1.  Ni vizuri ufahamu kwamba KABLA HAUJAZALIWA Mungu alishakujua na aliweka tayari KUSUDI,  NYAKATI, na UWEZO ndani yako maalum kwa ajili ya KANISA.{Yeremia 1:5; Zaburi 139:13,15,16;}


Kijana unatakiwa ujue Kusundi ambalo Mungu amekuitia Kama Ni kuimba imba Kama Ni uchungaji uinjilist Tumika Kwa Kujitoa Kweli Kweli Usiishi maisha ya Kikristo bila kujua Kusundi lako


2. Tambua kuwa hakuna Rika lililopewa upendeleo na nafasi ya pekee kama UJANA katika Ufalme wa Mungu.{Mithali 20:29; 1Yohana 2:14; Maombolezo 3:27}


Kijana Ni wazi Utambue Mungu amekupendelea Kuwekeza ndani Yako ukakamavu Ushawishi Kujitambua na Kujenga hoja zenye mashiko kwa Jamii na Kwa Kanisa Simama uelewe ujana wako Ni wa thamani


3. Licha ya uzuri mwingi ulioko kwenye UJANA, UJANA ni kipindi cha MPITO i.e. UMEPIMWA KWENYE MUDA na kwa hiyo basi UJANA HUPITA UPESI.{Mhubiri 12:1; Yohana 21:18;Matendo 17:26;Mhubiri 3:1,11}


KIJANA Utambue Rika la ujana utapita Sasa unaandaaje maisha Yako kiroho na Kimwili ukipita muda uliokuwa na nguvu ya Kumtumikia Mungu nakufanya kazi Yake wewe nakuacha ujihoji nguvu zako za ujana wako zinatumika kwa Mungu au dunia


4. Kijana ni KIUNGO MUHIMU SANA katika mwili wa Kristo yaani KANISA hivyo ni vema utambue thamani na nafasi yako katika kujenga na kuimarisha KANISA i.e. Mwili wa Kristo.{Waefeso 5:23; 1Korintho 12:27;Waefeso 4:12,16}


Kijana utawaleta na kuwavuna wengi utakapotambua nakuelewa Kuwa wewe Ni kiungo Kikubwa katika Kazi ya Bwana Nafasi Yako Ni ya mhimu ndani ya kanisa


5. Udhaifu na Ulemavu wa KANISA LA LEO ni matokeo ya VIUNGO vingi kulala na kutofanya kazi ipasavyo, na hasa VIJANA. {Mithali 25:14;}


Kijana Usilale au Kujiweka nyuma katika majukumu ya Kanisa Hebu amka Ufanye kazi Kama Mimi Baba Yako wakiroho Pastor Richard


6. Kijana anayeweza kuleta MABADILIKO kwenye KANISA ni Yule ambaye tayari ametambua thamani na nafasi yake kama kiungo katika MWILI wa KRISTO yaani KANISA, na anatumika katika kiwango na muda husika /sahihi {Yohana 4:34}


Kanisa ili Liendelee nakukua huhitaji Vijana wengi waamke wafanye Kazi ya Bwana wapewe kipa umbele ndani ya Kanisa


7. Ili Kijana Mkristo atumike vizuri kwenye KANISA ni lazima ajifunze kutoka kwa Yesu. Yesu ni mfano bora wa kuigwa na kielelezo sahihi cha maisha kwa Kijana yeyote.{1Yohana 2:6; Yohana 13:15;Mathayo 12:30;Mathayo 11:29}


Kijana chukua Siku moja TU ujifunze kwa Yeremia Daudi Samweli KWANINI wao waliweza Kumtumikia Mungu nakutembea ndani ya Kusundi la Mungu Kisha chukua hatua maisha Yako kuyajenga Kiroho na Kimwili. Mimi Ni Kijana mwezio rafiki Yako Mpendwa 


UKIWA KAMA KIJANA WAJIBU WAKO NI NINI NDANI YA FAMILIA.
Mambo ya kuangalia ili uwajibike sawasawa na mapenzi ya Mungu.                                                                                                                                
 (i) Ijue hali ya Familia yako. –maskini au tajiri, kabila lenu  katika upande wa mila na desturi.
(ii) Ijua haiba  ya wazazi wako  na ndugu zako. Kama ni sanguine, melancholic, flegimatic na choleric.
(iii) Tambua mila na desturi  za jamii inayo wazunguka. mafamo, baadhi ya makabila ni wakali sana, pia makabila mengine ni waongeaji. Ukiyatambua haya naamini utajua  ni jinsi  gani ya kuishi vyema bila makwazo yeyote na utapata ufahamu wa kuwa msaada mkubwa wa kuwasaidia  ndugu zako.  Mfano: Yusuph aliwatambua  ndugu  zake na baadaye aliwasaidia. Mwanzo 37:1-5
MUHIMUHata kama utafanikiwa  heshimu wazazi wako na ndugu zako.
''Waheshimu baba yako na mama yako; amri hii ndiyo amri ya kwanza yenye ahadi.'' Waefeso 6:2
Usilipe ubaya wowote anaye lipa ubaya ni Mungu mwenyewe,wakati wote kuwa mtu wa kusamehe. ,1petr 2:17, kut 20:12, mith 13:1.
Jambo la muhimu la kujua,jamii yako hukudharau kwasababu kugundua kilichopo ndani yako ni vigumu mno. ''Wakachukizwa naye. Yesu akawaambia , nabii hakosi kupata heshima, isipo kuwa katika nchi yake, na nyumbani mwake mwenyewe.'' Mathayo 13:57

    UKIWA  KAMA KIJANA WAJIBU WAKO NI NINI NDANI YA KANISA.
Kijana katika Biblia takatifu ameelezwa kama, ''Mtu awaye yote asiudharau ujana wako, bali uwe kielelezo kwao waaminio, katika usemi na mwenendo, na katika upendo na imani na usafi.''1Tim 4:12         
 Kama kijana usijidharau wewe ni wathamani sana jikubali mwenyewe.
   ''Jitahidi kujionyesha kuwa umekubaliwa na Mungu, mtenda kazi asiye na sababu ya kutahayari, ukitumia kwa halali neno la kweli.'' 2Tim 2:15

Tambua kwamba vijana ndio walio leta mapinduzi makubwa katika kanisa la kwanza.  
Mambo ya Muhimu ya kuyafahamu
  (i) Jikubali wewe binafsi. Usijizalau  na kuona huwezi kutumika. 2Tim 2:15 -16    
 Wewe ni mzuri  kwasababu Mungu ndiye aliye kuumba hivyo ulivyo.
Zingatia: kila asubuhi jiwekee ratiba ya kumshukuru Mungu kwa jinsi hivyo ulivyo. 

(ii) Acha mizaa kabisa.
 ''Heri mtu yule asiyekwenda katika shari la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.'' Zaburi 1:1.  
    
MUHIMU: Acha mizaa na jinsia tofauti kwasababu jinsia tofauti ni hasi na chanya pale zinapo kutana lazima matokeo yatokee.''Wala msimpe Ibilisi nafasi.'' Efe 4:27

ZINGATIA
: unapo luhusu mizaa katika maisha yako, shetani hupata nafasi ndani ya moyo  wako.    
''Wala si ajabu, Maana shetani mwenyewe hujigeuza  awe mfano wa malaika wa nuru.''2kor 11:14

 (iii) jigundue uwezo wako binafsi katika mwili wa kristo
 Katika huduma tano zilizopo ndani ya kanisa jitahidi kujua  upo kwenye nafasi gani.
Je, wewe ni mchungaji, mwalimu, mwinjilisti, mtume na nabii. Pia jambo lingine la msingi la kifahamu ni kwamba kuna karama za Roho Mtakatifu zipo Tisa. 1kor 12:4

Nazo ni (i) KARAMA ZA UFUNUO. Ambapo ndani yake zinapatikana hizi tatu ;- Kunena, kutafsiri na Unabii.
         (ii) KARAMA ZA UFUNUO. Ambapo ndani yake zinapatikana hizi tatu ;- maarifa, neno la heekima na kupambanua roho. 
         (iii) KARAMA ZA  NGUVU.Ambapo ndani yake zinapatikana hizi tatu ;- Imani ,Uponyaji na matendo ya miujiza.
  Baada ya kupata ufahamu ju ya karama na huduma, tambua karama ni kifaa kinachowezesha huduma ikue . 
     MUHIMU: usibahatishe huduma yako.       
Kwahiyo kutimiza wajibu wako ndani ya kanisa Lazima utembee katika kusudi la Mungu.''Kwa kadiri ya kusudi la milele alilolikusudia katika kristo Yesu Bwanawetu.'Efe 3:11

     Vitu vya kuzingatia unapo chagua mahali pa kumwabudu Mungu ukiwa ugenini.
  • Ondoa mtizamo mgando wa kimadhehebu, tambua kanisa la kristo wote ni mwili mmoja.
  • Omba kwa Mungu akusaidie kukuongoza mahali sahihi. 

UKIWA KAMA KIJANA WAJIBU WAKO NI NINI NDANI YA NCHI.          
Tambua kwanza kuwa kanisa ndilo linalo ongoza nchi, kanisa likiharibika nchi nayo imeharibika.
Mungu anapo angalia nchi huangalia kanisa kwahiyo kama tulivyo angalia kama kijana, una umuhimu mkubwa sana ndani ya kanisa na nchi kiujumla.

Wajibu wako ni nini. 
(i)bidii katika masomoMith 4:13
(ii) bidii katika shughuli zako zote mfano, mashambani,maofisini, hii itakuwezesha kuwajibika vizuri katika Taifa .1Samweli 13:1,9-11.


MAMBO MAWILI YA MUHIMU KWA KIJANA
*    Kama kijana ombea Taifa kwa mzigo na ufanye kazi kwa nguvu, akili na moyo wako wote.
*    Kama kijana kila mwisho wa mwaka laziam ufanye tathimini ya mipango yako uliyo weka unapo anza mwaka.
🦄🦄🦄🦄🌴🌴🌴🍇🍇🍇🍈🍉🍉🍉🍉🍉🍉🍉

MAMBO HAYA YA KUFANYA KUTIBU TABIA HATARISHI YA VIJANA WAKO

Fuata zoezi hili kuweza kutibu tabia isiyokubalika au hatari kwa watoto wako:


Mpe mtoto wako karatasi na kalamu, na pia kila mshiriki wa familia.


Kila mwanachama wa familia anapaswa kuchora nguzo nne kwenye karatasi.


Nguzo zinapaswa kuandikwa kama; masuala yanayokubalika, yasiyokubalika, makubwa na madogo.


Linganisha maonyesho yako na maonyesho ya kila mshiriki wa familia yako. Hii itakupa maoni ya tabia zipi wanaona kuwa zinakubalika na hazikubaliki.


Wakumbushe kwamba kila wakati watalazimika kujihusisha na shida kubwa, ngumu na kubwa wakati bado wanategemea wewe. Matokeo ya shida ni kwa kila mtu.


Shida kubwa ni pamoja na: kuvuta sigara, kunywa pombe, kuiba, dawa za kulevya, ngono, ponografia, uwongo, tabia mbaya, n.k.Ingawa tabia yoyote ambayo inaweza kukufanya ujisikie vibaya katika familia inaweza kuzingatiwa kama tabia isiyokubalika ambayo lazima ishughulikiwe na kila mtu kujua ikiwa ni nyingi au inaweza kupumzika.


Naitwa Pastor Richard

Morogoro veta Dakawa

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

NDOTO 20 ZA SHULENI TU MAZINGIRA Ya SHULE

SOMO: NGUVU YA KUJITAMBUA

SOMO:ADUI NA JINSI YA KUMKABILI ADUI YAKO.