SOMO:Jua Njisi Ya Kuvua Utukufu wa Shetani nakuvaa utukufu wa Mungu
⌚🌅🌠SOMO: MVUA UTUKUFU wa SHetani___ VAA UTUKUFU wa MUNGU.🔥🌠🌠
Vitabu: Mathayo;16;27 Mathayo:25:31 Yohana;9;24 Warumi:5;2
Isaya;60;1_5
Lengo La SOMO; Kukujulisha kujua nguvu ya UTUKUFU wa MUNGU ndani yako na njisi ya kuulinda utukukufu wa Mungu.
Karibu Naitwa Pastor Richard
UTUKUFU NI Nini?? Huwa Ni Nuru au mwanga unaokuwa unakuzunguka katika kuhakikishia unakutambulisha kwenye kazi unayoifanya.
Kwa mfano rahisi unaweza chukua zoezi hili
Nzima taa yako usiku halafu uone unazungukwa na Nini Kama utaona ngiza Ni utukufu wa Shetani unavyokuwa unakuzunguka kwa Kukosa Neno la Mungu ndio unajikuta mtu Anateseka na Tatizo bila kujua chazo kumbe kwa kuwa Anakuwa Yupo amefunikwa na UTUKUFU wa WANADAMU au Utukukufu wa Kumtengemea Hirizi waganga uchawi Miungu majini nk
Mtu aliyezungukwa na Hali ya ngiza huwa Ni kazi pia Kuelewa adui anayemtesa Yupo nae ndani au Yupo nae nje kwa kuwa taa Yake Huyu mtu ameizima Anaona ngiza TU kwa hiyo hata adui anavyokuwa anamtesa nakumuonea haoni sababu Yupo ngizani
UTUKUFU wa MUNGU
Hii huwa mfano wa Taa iliyowashwa Kwenye eneo palipo na ngiza humsaidia mtu kuona ndivyo hivyo mtu aliyeupokea au kuvaa utukufu wa Mungu mwenye taa inayowaka huwa analitawala ngiza hivyo hivyo mtu mwenye utukufu wa Mungu hutawala falme za ngiza na magonjwa Yake kwa kuwa Kila adui atakapokuwa Anataka Amshambulie Anamkuta Huyu mtu amezungukwa na Nuru Kama ilivyo katika uhalisia wa ngiza hupingwa nakuondolewa na Nuru.
Faida Unazopata Utakapoamua Kuvua ngiza Uvae Nuru
1;Mambo yako yataonekana.
2;Utaangaza Kila ufikapo utaonekana kwa watu Ni Bora.
3;Biashara na makapuni yako yataangaza nakuenea
4;Huduma yako itakuwa kubwa
5;Magonjwa wachawi mapepo nk hawatakutesa
6;Maisha yako kwa ufupi yataangaza na utaonekana.
HASARA UKiendelea Kuishi Maisha Bila UTUKUFU wa MUNGU.
1;Hutaoneka na Mambo yako hayataangaza popote hata mtaani kwako tu mwenyekiti hatakujua.
2;Biashara Kampuni zako Zitakuwa za eneo hilohilo au kufa kabisa
3;Utateswa na mapepo majini wachawi
5;Maisha yako utakuwa unapigwa na Kila Uadui kiroho na kimwili Hali itakayokufanya wewe uteseke
UFANYE NINI SASA ILI USITESEKE.
1;Mpokee Yesu Kama bado
2;Lazima ulelewe kiroho upende kuandika nakufatilia Neno la Mungu
3;Unatakiwa uwe na Madhabahu na Baba wa Kiroho hapo ndipo utashiriki kutoa Fungu lako la kumi usitoe Kila Madhabahu.
4:Penda kusoma Vitabu vya Neno la Mungu na Mafundisho mbalimbali yatakufungua
UTAKAPOKUWA NA Neno la Mungu Utakuwa Umefaulu Kila kitu
Simu Ya Pastor +255759861768
Maoni
Chapisha Maoni