SOMO:$ifa 7 Mwanamke Mpambanaji
SOMO; SIFA 7 MWANAMKE MPAMBANAJI Karibu katika Darasa Hili ujifunze na ujue Sifa za mwanamke mpambanaji Naitwa Pastor Richard Mwalimu wa WANANDOA 1;Jasiri Mwanamke mpambanaji ni jasiri anaona nafasi za kujiendeleza na kuzinyakua haraka. Mwanamke jasiri haogopi kushindwa na changamoto zilizo mbele yake, siku zote huchagua kuzikabili. Wanawake wengi majasiri wamefanikiwa kuinua uchumi wao na kuzisimamia familia zao, wakati mwingine bila hata ya msaada wa mwanaume. Ni wajasiriamali. Ni wanawake wenye nyadhifa za uongozi wakifanya kazi na kuleta maendeleo kwa bidii. 2;Hufanya Maamuzi Sahihi Mwanamke mpambanaji haogopi kufanya maamuzi sahihi juu ya maisha yake na kufuatilia mipango yake. Hupokea maoni chanya na kuamua pia kupuuzia maoni ya watu wengine yasiyo na tija ama ambayo hayamsaidii kwenda mbele na kutimiza ndoto zake. Kutokana ma mapito yake, mwanamke mpambanaji hufanya mamuzi sahihi juu ya jinsi gani ya kubadili mwenendo wa maisha yake ili kujibores...