SOMO:USHINDI WA PASAKA
Somo: Ushindi Wa Pasaka: Kutoka Gizani Kwenda Nuruni Ninayekukaribisha Somo hili Ninaitwa Pastor Richard Wa Morogoro Nataka Tukumbushane Umuhimu Wa Sikukuu ya Pasaka Lengo la Somo: Kuelewa maana halisi ya kifo na ufufuo wa Yesu Kristo na jinsi unavyompa mwamini mamlaka na matumaini mapya. Nimeligawanya Somo hili Mara Tatu Ili Kukufanya Uelewe Vizuri 1Alhamis Kuu:- Hii hutukumbusha kuwa wanyenyekevu na Wenye upendo 2:Ijumaa Kuu:- Hii Hutukumbusha Gharama ya Ukombozi Yesu Alivyokufa Kwa Ajili yetu ili tuwe na ukombozi. 3:Jumapili Ya Pasaka:- Nguvu ya Ushindi wa Vizuizi vyote na vipigamizi Vyote. 1. Maandalizi na Unyenyekevu (Alhamisi Kuu) Kabla ya ushindi, kuna utii. Yesu alituonyesha kielelezo cha upendo na utumishi kwa kunawa miguu wanafunzi wake na kuanzisha Meza ya Bwana. Mstari wa Kusoma: Yohana 13:14-15 — "Basi ikiwa mimi, niliye Bwana na Mwalimu, nimewanawa miguu, imewapasa vivyo hivyo kunawana miguu ninyi kwa ninyi." 2. Gharama ya Ukombozi (Ij...